kama hujui ulikotoka huwezi kujua mahali ulipo wala sio rahisi kutambua wapi unaelekea japo unaendelea kupiga hatua kuelekea usikokujua mwisho wa siku unajikuta umerudi pale pale.
Ni wakati wa vipofu kuona jua na viwete kutembea baada ya miaka 50 tangu wazaliwe na kufungiwa ndani kama watu wasiojiweza wakati wengine wanamagari, majumba ya kisasa na kufanya biashara kubwa hapa nchini.
Nikisema niwakati wa mabadiliko halisi wapinga maendeleo watasema ujana unamsumbua na waliotufirisi watasema anatuonea wivu kisa tuna pesa nyingi.
Mimi sio mwanasiasa wala mwanaharakati kana kwamba natetea kambi rasmi inayolenga kulenga mabadiliko ya kisiasa yatakayo badili mfumo mzima wa utawala, uchumi na jamii kwa jumla bali mimi ni mtanzania niliyechoshwa na utawala usioonyesha njia ili watu wake wasonge mbele.
Najisikia kichefuchefu ila oktoba 25 lazima nikatapike kwa sababu wamewatesa wazee wetu bado wanaendeleza mchezo wao mchafu wa kulifanya taifa hili la kwao na kutufanya wengine wahamiaji tu.
Watanzania tusipoleta mabadiliko mwaka huu ,tupelekwe India kwa matibabu ya akili maana hapa nyumbani hatuna madaktari kisa watawala wanauwezo wa kuwafuata nje ya nchi. Aibu kubwa japo wao wanafurahia tu.
Siasa inaendesha uchumi ambao hujenga jamii bora ya kitanzania. Mfumo wa siasa ya Tanzania ni duni hivyo tunahitaji mabadilko.
TASWIRA YA MABADILIKO KWA VIJANA.
Vijana wako mstari wa mbele kuona kwamba taifa hili linakombolewa upya kutoka mikononi mwa waliopewa uhuru 1961 ndio maana hawaoni uchungu wa kuiendeleza taifa lao kwa manufaa ya watanzania wote.
Kazi kubwa imefanywa na vijana waliopata nafasi ya kuingia katika vyombo vya maamuzi na kuongeza uelewa wa kisiasa na utawala wa nchi hii kwa vijana wenzao.
Ni Dhahiri kwamba vijana wakielimika ndio chachu ya mabadiliko kila sehemu haijalishi ni katika hali gani (vijana ndio dira ya maendeleo).
Wenye upeo mdogo wa kufikiri(samahani kwa neno hili kali) wanasema bado siasa ya nchi yetu inaenda vizuri na taifa linakuwa kwa kasi sana, haina haja ya kubadili mfumo wa kiutawala(I feel sorry if you are the one)
Lakini kuna vijana wanaotaka kuwaonyesha watawala kuwa taifa hili ni la wote na halistahili kuwa katika hali hii.
Lazima niwe wazi katika hili , vijana wakitanzania wamehamasika na wameamka  kushiriki katika siasa za nchi hii ,hapana shaka mabadiliko yanakuja.
TASWIRA YA MABADILIKO KWA WANAWAKE
Mwanamke anapenda maendeleo ,hata katika nyumba mwanamke anapenda kununua vitu vyenye thamani na vyenye kuvutia lakini ni muoga wa kufyeka njia itayoleta maendeleo.
Wakati mtazamo wa vijana ni kubadili mfumo wa kisiasa hapa nchini wanawake wamekuwa nyuma kidogo kutokana na hofu ya kuleta mabadiliko yatayoleta mageuzi ya kiuchumi wetu na kijamii.
Wengine wanaona hakuna sababu ya kuleta mabadiliko kwa sababu wanaona hata baada ya kubadili mfumo wa utawala kazi yake ya kuoka mikate, mama ntilie itaendelea. Hivyo basi wanaona kwa nini nipigane kuleta mabadiliko?(uelewa  mdogo wa siasa/political understanding is very limited most of the women).
Wako wanawake wanaoona kutaka mabadiliko katika taifa hili ni uhuni unaotaka kufanywa na vijana na huenda kukatokea machafuko ambapo wanawake wanakuwa wahanga (fikra potofu). Lakini hawaridhishwi ni mfumo uliopo.
Wengine wanasema tukiwapigia kura wanaotaka mabadiliko watakuwa kama hawa hawa , kwa nini nihangaike kuleta mabadiliko(kuishi kwa mazoea na kushindwa kufikiri maisha ya badae).
Hapana shaka nikisema naona Tanzania mpya inakuja ,kufikia hapa lazima niunge mkono mabadiliko.Hawa watu wakibaki wataongea sana tena kwa dharau na kuendeleza ukandamizaji kwa raia.
TASWIRA YA MABADILIKO KWA WANAUME
Kwa asilimia kubwa wanaume wanauelewa mkubwa wa siasa, lakini wamegawanyika katika makundi mbalimbali kulingana na mahitaji ya mtu husika.
Wapo wanaume wenye taswira waliyonayo wanawake kuhusu mabadiliko kutokana na kukosa elimu ya kujitambua na uelewa mdogo wa siasa za nchi hii (Baadhi ya wanaume wamekosa ujasiri kuleta mabadiliko na wengine wanaona maisha tunayoishi ni halali yetu)…….badilika kabla ya octoba 25/be strong.
Lakini pia kuna wanaume wanaofaidika na mfumo wa utawala uliopo, japo wanaona kuna kila dalili na umuhimu wa kubadili mfumo, wao wameziba masikio kana kwamba hawasikii vilio vya watanzania (conservative).
Kuna kundi kubwa la wanaume kwa sasa linataka mabadiliko kwa sababu wengi wao wanateseka na kunyanyaswa na mfumo huu usiofaa. Kuna makundi ya wakulima(ruzuku) , madereva(leseni), walimu(Mishahara), wafanyabiashara(EFD)….mabadiliko ni lazima/change is inevitable.
MAAJABU YA TANZANIA YANAYONIFANYA NIHITAJIA MABADILIKO.
-Tanzania ni nchi pekee ambayo viongozi wanagawana pesa za umma na viongozi ngazi ya juu wanacheka na wengine wasaidiana ili mwenzao asikamatwe (ujinga).
-Tanzania ni nchi pekee ambayo 1.6Bil- ni pesa ya mboga na 400mil- ni vijisenti (dharau).
-Nchi ambayo wananunua bidhaa lakini hawataki kurudishiwa chenji hadi mwenye duka akuletee(kutojali)
-Nchi yangu hupati kazi bila kuwa na ndugu , rafiki au jamaa labda uwe mwalimu(umimi).
-Nchi ambayo mwalimu wa primary ni yule aliyefeli form four
-Wanafunzi wanakaa chini wakati kuna misitu kibao
-Nchi ambaye wananunua ndege ambaye haiwezi kuruka na hakuna wa kuwajibika(wanahisi hatuelewi)
-Nchi ambayo mabasi yanaletwa lakini milango iko kinyume na kituo na hakuna anaewajibika au kuwajibishwa.(umakini)
-Nchi ambayo unaumwa kichwa unapasuliwa goti(umakini) but who care?
-Nchi ambayo waleta maendeleo wanafutwa katika ramani ya dunia.
-Nchi ambayo polisi anajua haki za raia kuliko raia mwenyewe(elimu ya kujitambua hakuna).
-wanawake wanajifungulia njiani hata akifikishwa zahanati hamna wahudumu wala vitanda vya kulazwa, (nani akujali wakati wake zao wanajifungulia marekani).
Kwa kifupi hii ndio nchi yangu ambayo kila kitu tunaletewa kutoka nje wakati tuna kila kitu kinachoweza kutufanya tuwe watengenezaji wa bidhaa mbalimbali na kuziuza nje ya nchi.
Utasema nini watu wanafanya biashara ya malori wewe raia unataka reli ya kati itengenezwe?  kama unadhani majangili ni raia wa kawaida basi umenoa, kwa ulinzi na usalama wa nchi hii mtu angewekwa ndani kesi zingekuwa on fire now.
TANESCO inakata umeme wiki tatu ,nani anajali? Au nani amewajibika? Fimbo yako kura yako ,tuwachape octoba 25(watanzania wanapoteza mamilioni ya pesa kutona na kukatika kwa umeme)
Maji hayatoki katika nchi iliyobarikiwa mito ,maziwa na bahari(tuwaonyeshe octoba 25, binafsi nimewachoka hawa wadudu).
Mpoto anasema kukumbatia hewa kama mti ni ujinga, mimi nasema heri debe tupu kuliko sifuri. Lakini maandiko yanasema mti usiozaa matunda ukatwe na uchomwe moto,Bwana asema.
Wacha tuseme ukweli hata Musa alikuwa anaishi Misri lakini aliwakomboa wanaisraeli japo hakufika Kanani lakini Joshua aliwafikisha na wakawa huru.
TWENDE TUKAPIGE KURA.
TIME FOR CHANGE, NO MATTER WHAT!




(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({});

0 comments:

Post a Comment

 
Top